Amesema Yarasuli, maneno yalo muruwa,
Tena ambayo ni kweli, matamu kama haluwa,
Kwa Jamila na Jamali, bila hata kubaguwa,
Mapenzi zinazidisha, zawadi mkipeana.
Waja inasitahili, kufanya bila ya ngowa,
Na wala si ukatili, jambo la kusisimua,
Toa bila ya ukali, wala hutopungukiwa,
Mapenzi zinazidisha, zawadi mkipeana.
Uondoshe ubakhili, hilo jambo ukijuwa,
Usihofu yako mali, kwa zawadi kuitowa,
Kabana yake Kabuli, kingi utazidishiwa,
Mapenzi zinazidisha, zawadi mkipeana.
Usione mushikeli, bali jambo lilo sawa,
Ukaufanya muhali, hodari wa kuvumbuwa,
Ni akiba iso mbali, nawe wajakutendewa,
Mapenzi zinazidisha, zawadi mkipeana.
Wema huwa ahu'feli', nahau yangu dokowa,
Bora huu muhimili, upende kama mauwa,
Weka kwenye jeduwali, fakiri na wenye hatuwa,
Mapenzi zinazidisha, zawadi mkipeana.
Beti sita kituoni, mbele sitoendelea,
Amini usiamini, wasia huu mbolea,
Tena ulio yakini, Mtume aloongea,
Mapenzi zinazidisha, zawadi mkipeana.
Siri Zangu | Swahili Net | Swahili Fire | Mapenzi Ngono na Ndoa
Thursday, April 21, 2011
Mashairi Kutoka Tanzania:Zawadi
Posted by
Igihozo
at
11:32 AM
Labels:
mashairi ya kiswahili
Newer Post
Older Post
Home
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
CelebSense
Loading...
0 comments:
Post a Comment