Bismillah naanza, jina la Mola Karima,
Mjuzi alotufunza, kwa Wahay na ili hama,
Na Mitume kwa kujaza, yalomema na harama,
Yarabi tupe elimu, tupiganie Isilamu.
Iqraa inasema, wajibu sote kusoma,
Si kwa baba si kwa mama, kusoma kufanya hima,
Uingereza Panama, kote twendeni kusoma,
Yarabi tupe elimu, tupiganie Isilamu.
Islamu ni elimu, shime nawahusieni,
Muhammad wa Adamu, wote watu taalamani,
Hima hima Isilamu, tujitoe ujingani,
Yarabi tupe elimu, tupiganie Isilamu
Elimu kwetu faradhi, yatangulia hata sala,
Elimu kwetu ni hadhi, japo Isilamu twalala,
Qur'an na Hadithi, kote elimu melala,
Yarabi tupe elimu, tupiganie Isilamu
Enyi mlo mashuleni, elimu piganieni,
Hata kufia mezani, kwenu jitahidini,
Ameahidi Manani, peponi kuwaficheni,
Yarabi tupe elimu, tupiganie Isilamu.
Hala hala wanafunzwa, elimu si ya kuchezwa,
Hata Mtume ajuzwa, kwa kubanwa na kutunzwa,
Hata wale walojuzwa, kwahilo walihimizwa,
Yarabi tupe elimu, tupiganie Isilamu.
Kaditama namaliza, husiya walomaliza,
Tumieni mlojuzwa, ondosheni umma giza,
Qiyama waja ulizwa, manufaa ya kujuzwa,
Yarabi tupe elimu, tupiganie Isilamu.
Mwanawetu Hamza (Mujahidat),
Dar es Salaam
Siri Zangu | Swahili Net | Swahili Fire | Mapenzi Ngono na Ndoa
Thursday, April 21, 2011
Mashairi Kutoka Tanzania:Yarabi tupe elimu
Posted by
Igihozo
at
11:27 AM
Labels:
mashairi ya kiswahili
Newer Post
Older Post
Home
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
CelebSense
Loading...
0 comments:
Post a Comment